Monday, 16 September 2013
Sunday, 19 May 2013
Vipashio vya lugha
Lugha ina vipashio vinne navyo ni kama vifuatavyvo:
1 Sauti
2 Mofimu/silabi
3 Neno
4 Sentensi
Mofimu ndicho kipashio kidogo sana cha lugha. Sauti huunda silabi. Silabi ni mpigo mmoja wa sauti unapotamka. k.m neno sentensi lina silabi tatu, nazo ni se-nte-nsi. Kama inavyoonekana, 'sentensi' ni neno ambalo limeundwa kwa silabi tatu.
Naam, sauti ikishaunda silabi, silabi ikaunda neno, neno nalo linaunda nini? Tuone mfano wa maneno yafuatayo hapa chini:
Sentensi hii haisomeki vizuri.
Sentensi hii hapa juu imeundwa kwa manano manne: sentensi + hii + haisomeki + vizuri. Hivyo basi tunapata kuwa neno au maneno yanaunda sentensi. Yaani sentensi ni neno au fungu la maneno yanayobeba ujumbe uliokamilika, na sentensi ndicho kipashio cha juu sana cha lugha
1 Sauti
2 Mofimu/silabi
3 Neno
4 Sentensi
Mofimu ndicho kipashio kidogo sana cha lugha. Sauti huunda silabi. Silabi ni mpigo mmoja wa sauti unapotamka. k.m neno sentensi lina silabi tatu, nazo ni se-nte-nsi. Kama inavyoonekana, 'sentensi' ni neno ambalo limeundwa kwa silabi tatu.
Naam, sauti ikishaunda silabi, silabi ikaunda neno, neno nalo linaunda nini? Tuone mfano wa maneno yafuatayo hapa chini:
Sentensi hii haisomeki vizuri.
Sentensi hii hapa juu imeundwa kwa manano manne: sentensi + hii + haisomeki + vizuri. Hivyo basi tunapata kuwa neno au maneno yanaunda sentensi. Yaani sentensi ni neno au fungu la maneno yanayobeba ujumbe uliokamilika, na sentensi ndicho kipashio cha juu sana cha lugha
Subscribe to:
Posts (Atom)